mwanasoka bora kabisa kwa sasa katika dunia ya soka Lionel messi jumanne hii ameshindwa kabisa kuwanyanyua mashabiki wa timu yake ya Barcelona ilipokuwa inakipiga na Inter milan ya Italia katika dimba la Giussepe meazza.katika mechi hiyo iliyomalizika kwa wenyeji Inter milan kushinda kwa jumla ya mabao 3-1..magoli ya Inter milan yalifungwa na Diego milito,wesley sneijder na douglas maicon wakati bao la Barcelona liliwekwa kimiani na pedro rodreguez kiungo wa kimataifa wa spain
No comments:
Post a Comment